Wakati mkoa wa Dodoma ukiendelea
kukua kwa kasi kufuatia kuboreshwa kwaMiundombinu na ujenzi wa kituo cha
mabasi yaendayo mikoani pamoja na ujenzi wa stendi ya Daladala maarufu kama JAMATINI umekuwa ni chanzo cha
msongamano wa magari,abiria,wafanya biashara na vibaka hali ambayo nikero kubwa
kwa wakazi Mkoa wa Dodoma. Mwandishi wetu alipozungumza na SUMATRA wao walisema:Tuliweka utaratibu mzuri wa daladala
zilizohamishwa kutoka Jamatini nakwenda eneo la Reilway ilikupisha ujenzi wa
kituo hicho cha daladala na mabasi yaendayo mikoani wao walipelekwa NANENANE sasa kama hawa wa mabasi
yaendayo mikoani wamerudi eneo walipo hamishwa watakuwa wamekaidi agizo la
Serikali. Tulipozungumza na madereva wa mabasi yaendayo mikoani kwanini wamerudi eneo
waliloondolewa wao walijitetea kwa kusema: Wametupeleka NANENANE pasipo kutuandalia mazingira
kule hakuna huduma za kijamii abiria wanaonabora wsafiri na mabasi ambayo
booking office zao zipo mjini kwahiyo sisi tuliopo nanenane tunakosa abiria
ndio maana tumeona bora tuje tukomae hapa angalau abiria si haba. Abiria kilio
cha kikubwa ni wezi wa mifukoni ambao wanawakosesha amani. Pia wafanyabiashara
hususani MAMA NTILIE wamekuwa wakifanya biashara zao kwenye mazingira hatarishi. HII NDIO DODOMA LAZIMA TUKUBALI SHIDA ILI
IWE NA MUONEKANO WA MAKAO MAKUU YA TANZANIA. KWA HABARI NA MATUKIO TEMBELEA
Na Mwanahabari wako ABDUL RASHID MUSSABURUDANI MAKINI
No comments:
Post a Comment