Monday, March 11, 2013

MGAO WA UMEME UNAOTESA WANANCHI MBALI NA KUPUNGUZA MAPATO YA TANESCO


Wananchi wa mkoa wa Dodoma wamewalilalamikia shirika la umeme Tanzania TANESCO Kuwa pamoja na adha wanayoipata kutokana na mgao wa umeme ni hasara kwao pia ni hasara kwa Tanesco kwani wanapo kata umeme wanapunguza matumizi ambayo hupelekea kiwango kidogo cha manunuzi ya LUKU na malipo kidogo ya bili. Kwa upande wa wanachi wengine wao walisema:sisi tunategemea umeme kujipatia kipato cha kila siku kwa mfano sisi tunao chomelea, watu wa salon,na watu wengine ambao bila umeme hawawezi kufanya kazi umeme unapokatika kwetu ni hasara kubwa.

Tulibahatika kuzungumza na meneja wa TANESCO yeye alisema:Nikweli mgao wa umeme unapunguza mapato ya shirika kwa kiasi kikubwa. Pia akaendelea kwa kusema hata wao hawapendi kuweka ratiba ya mgao ila ina walazimu kutokana na hali halisi ya kina cha maji kilichopo MTELA.Akamalizia kwa kusema mgao si zoezi la kudumu litakwisha ndani ya kipindi kifupi. MGAO WA UMEME NI ADHA INAYOENDELEA KUWAKUMBA WAKAZI WA DODOMA.        BURUDANI MAKINI    
 KUTOKA SHAZI USWAZINI NI MIMI MWANAHABARI WAKO:  
ABDUL RASHID MUSSA
PIA UNAWEZA KUPATA HABARI HIZI KUPITIA     ACCOUNT YA FACE BOOK/CRAYZ BEEZ

No comments:

Post a Comment