Monday, March 11, 2013

MANISPAA WAENDELEA KUWANYANYASA WAFANYABIASHARA WADOGO WA DODOMA






Waliwavunjia soko la RAILWAY wakaenda nje ya soko la MAJENGO baada ya kuwafukuza wakahamiSABASABA na usiku wa kuamkia leo wamewavunjia na kusababisha hasara kubwa kwa wafanyabiashara hao.  Wakizungumza na SHAZI USWAZINI wafanyabiashara hao walikuwa na haya ya kusema: Manispaa wanatunyanyasa sana na hii ni kwa sababu walipo tuvunjia Railway wakatupeleka CHADURU sehemu ambayo ni kando ya mji na kama unavyojua biashara zetu zinahitaji sehemu yenye mkusanyiko wa watu. Tukaamua tukabanane soko kuu Majengo walipo tufukuza tulienda kwa mkuu wa mkoa kulalamika ndipo Manispaa wenyewe wakatuleta hapa sabasaba chaajabu usiku wa leo wametuvunjia bila taarifa. Pia licha ya kuharibiwa kwa bidhaa zao wanadai bidhaa zilizo haribiwa ni chache bidhaa nyingi zimeibwa. Mwandishi wetu alijitahidi kumtafuta Mkurugenzi wa Manispaa lakini hakufanikiwa kumpata. HAYO NDIO YALIOWASIBU WAFANYABIASHARA WA ENEO LA SABASABA(DODOMA MJINI).




Nikweli Serikali Ina Nia Njema Na Wanainchi Wake? Ukizingatia Soko La Ajira Ni Gumu Katika Nchi Yetu.Wananchi Wanapojiajiri Inakuwa Vita Kati Yao Na Serikali..... Je Nini Kifanyike???  Unaweza Kututumia Maoni Yako  Kupitia Account yetu ya facebook/CREYZ BEEZ..



Na Mwanahabari wetu Abdul Rashid, kutoka Shazi Uswazini.

No comments:

Post a Comment