Friday, March 8, 2013

BOMOA BOMOA YAENDELEA KWA KASI DODOMA MJINI



Ilianzia NJEDENGWA ikahamia MBUYUNI hatimaye KIKUYU Na sasa kabla ya kwenda MJI MWEMA na NDACHI wameanzia CHINANGALI WEST na watamalizia na KWA MWATANO.

Wananchi wa mkoa wa Dodoma hususani manispaa ya Dodoma mjini imewalalamikia Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa kitendo cha kubomoa makazi yao kwa madai ya kuboresha mji. Baadhi ya wakazi hao walisikika wakisema CDA Wamekuwa wakibomoa makazi yao pasipo na kuwaonyesha makazi mengine ya kwenda kuishiKwa upande wa CDA tumezungumza na mkurugenzi wa CDA alijitetea kwa kusema “ Tuliwapa taarifa mapema wale wote walio vamia na kujenga kiholela waondoke baada ya miezi sita(6) 


Lakini walikaidi agizo hilo sasa hatuna budi kuwaondoa kwa nguvu” Na aliipo ulizwa kuhusu viwanja walivyo gawa kwa upendeleo alijibu: Mbuyuni ni eneo la viwanda hakuna mwananchi aliyegaiwa kiwanja Pia MJI MWEMA ni eneo la makaburi. Mwandishi wetu ali dodosa kujua malipo ya wakazi hao walio bomolewwa makazi yao. Alijibu: Barabara ya CHINANGALI WEST ilipimwa mwaka 1972/73 na hapa kuwa na makazi ya watu.Wenye haki ya kulipwa ni wale walio kutwa na barabara na si walio ikuta barabara. Pia wananchi wamekuwa wakiilaumu CDA kwa utapeli wa kuuza kiwanja kimoja kwa watu zaidi ya watatu kwa kusema huo ni wizi. POLENI SANA WAKAZI WA MAENEO YANAYO KUMBWA NA BOMOABOMOA .BURUDANI MAKINI   

No comments:

Post a Comment